Articles

Affichage des articles du février, 2022

SOMO KUHUSU MAJARIBU

Image
  USOMI  : 1 Wakorintho 10:12-13 I.    MAANA YA JARIBU: Jaribu ni kipimo cha imani kwa watu wote; na mwisho ya kujaribiwa kwako na ( Mungu, Shetani, Sifa au Cheo, Ahadi ya Mungu, Mwili yako yenye kutamani na Tamaa zitokazo katika Nafsi ya mtu ); ni mpaka kufa.  Jaribu halijawa jaribu, mpaka linamufikisha mtu kwenye njia panda; mahali pa kuamuwa kama ataacha Imani ya Yesu Kristo, kama ataacha alicho kuwa anafanya au akigojeye  au tena mtu aendeleye kuvumiliya ( yaani kuchukuwa maamzi sahihi ) . Na hicho ni kipindi kizito cha kukatisha sana tamaa!   II.     KAZI AU LENGO YA JARIBU MAISHANI MWETU  Kwa somo hili, tutagusia sana maana ya jaribu kwa Wakristo: - Jaribu inakuja kuandaa mukristo kupokea baraka, kuinuliwa au kupandishwa cheo; alakini ni lazima mtu huyo ashinde jaribu ndipo hayo yatajitokeza ( Yakobo 1:12 ), ( Kumbukumbu la torati 8:16 ); - Jaribu inamusaidia mukristo kutengeneza mawasiliano au mahusiyano (re...

KITU CHA KUFANYA UNAPO KUTANA NA MAJARIBU MBALIMBALI MAISHANI

Image
USOMI : 1 Wakorintho 10:12-13 I. KIINGILIO: Kumbuka kuna jambo ambalo unatakiwa kufanya kusudi uvuke hivyo vipindi viguma vya majaribu, hata kama Bwana ka ahidi tayari kufunguwa mulango ili jaribu lipite, sababu ya uaminifu wake; lakini katika kitabu cha Luka Mtakatifu sura 9:11 ; imeandikwa “... Yesu aliwaponya waliyo kuwa na haja ya kuponywa”. Na Mithili 8:17 nayo ina sema: “Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona” Tena Yeremiya 33:3 Bwana anasema: "Niite, nami nitakuitikia..." II. JAMBO LA KUFANYA   Jambo la kwanza: - Usimunungunikiye Mungu wala mwanadamu; sababu manunguniko huwa inarudisha ahadi ya Mungu nyuma. Mfano ya wana Waisraeli jagwani toka inchini Misri kwenda Kanani (Hesabu 14:34-38; 1 Kor. 10:10); - Chunguza sana maneno ya kinywa chako, ili usije ukakiri mazaifu wala kujilaani mwenyewe (Yakobo 3:10; Mwanzo 25:32 na Kutoka 30:19) . Tena jifunze pia kuchunga siri ya maisha au huduma yako; sababu Shetani ni mujanja sana, anazungukazung...