SOMO KUHUSU MAJARIBU
USOMI : 1 Wakorintho 10:12-13
I. MAANA YA JARIBU:
Jaribu ni kipimo cha imani kwa watu wote; na mwisho ya kujaribiwa kwako na (Mungu, Shetani, Sifa au Cheo, Ahadi ya Mungu, Mwili yako yenye kutamani na Tamaa zitokazo katika Nafsi ya mtu); ni mpaka kufa.
Jaribu halijawa jaribu, mpaka linamufikisha mtu kwenye njia panda; mahali pa kuamuwa kama ataacha Imani ya Yesu Kristo, kama ataacha alicho kuwa anafanya au akigojeye au tena mtu aendeleye kuvumiliya (yaani kuchukuwa maamzi sahihi). Na hicho ni kipindi kizito cha kukatisha sana tamaa!
II. KAZI AU LENGO YA JARIBU MAISHANI MWETU
Kwa somo hili, tutagusia sana maana ya jaribu kwa Wakristo:
- Jaribu inakuja kuandaa mukristo kupokea baraka, kuinuliwa au kupandishwa cheo; alakini ni lazima mtu huyo ashinde jaribu ndipo hayo yatajitokeza (Yakobo 1:12), (Kumbukumbu la torati 8:16);
- Jaribu inamusaidia mukristo kutengeneza mawasiliano au mahusiyano (relationships) mazuri kati yake na Mungu, kwa kuwa Mungu anafurahiya sana tunapo mushirikisha katika mambo yetu ndani ya maombi (Yer. 33:3; Mithali 8:17; 1 Petro 5:6-7);
- Jaribu inaimarisha sana Imani, Matumaini, Upendo pamoja na Uaminifu ya mkristo ndani ya Kristo Yesu (Kumbukumbu la Torati 8:2-4; Warumi 5:3-5; 1 Wakorintho 13:13).
III. NANI AWEZA AU NINI INAWEZA SABABISHA MAJARIBU KWA MWANADAMU NA KWA MALENGO GANI?
1) KWANZA: NI MUNGU MWENYEWE (Zaburi 105:16-20; Mwanzo 22:1; Kutoka 16):- Lengo la kwanza: kuandaa mwanadamu kwaaji ya mema, kuinuliwa utukufu hadi utukufu-Imani hadi Imani, kupokea karama au zawadi za roho mtakatifu; (Kumbukumbu la torati 8:2-4, 16). Ikumbukwe ya kwamba hakuna mfalme bila vita soma kitabu cha Waamuzi 3:1-4;
- Lengo la pili: kuamsha zamiri na kukumbusha mwanadamu agano na kusudi la Mungu kwake au njia Zake (Yer. 25:4-13; 2 Wafalme 22:19 ). Jaribu aina hii ni kwa watu wenye kuasi maagizo ya Mungu tunaweza sema tena kwamba ni azabu toka Mungu;
- Lengo la tatu: Jaribu kama ishara au tahazari (attention) kwa mwanadamu ili kumuepusha na shida mbalimbali, ikiwa hataki kusikiya shauri au maagizo (Kutoka 4:8-9; Ayubu 33:14,17; Hesabu 22:22-35).
Mfano 1: “Kuna muhuburi ambaye Mungu alisemesha akiwa anauza sokoni, aache kuuza na aende kutangaza neno lake ile siku; bahati yake aka tii sauti hiyo na akaenda, hata kama alikuwa bado haja uza hata kitu chochote kati ya byashara yake alio kuwa nayo. Mukutano wa injili ukaendelea na uwepo waajabu, ukamalizika nyuma sana saa za kufunga soko. Papo hapo, nvua kali ikatokea na hana hata pesa za kulipa gari ili arudi nyumbani, sababu hakupata muda wakuuza; akamuomba Mungu akimukumbusha kazi aliyo mufanyiya mchana muzima, tena byashara alivyo navyo haviwezi vumiliya kurowana; yaani bikirowana tu na binaharibika byote. Ingawaje maombi, Mungu akawa kama hamusikiye, nvua ikaendelea kunyesha wakati mtumishi akiwa njiani na byashara yake kichwani mpaka byote bika rowana hata kuharibika; akaenda nyumbani akimunungunikiya sana Mungu sababu alimuomba nvua isiharibishe byashara yake ila Mungu hakumujibu sawa sawa na ngisi alivyo muomba.
Wakati akiendelea, karibuni na kwake kulikuwa pori, akasikiya ndani ya ile pori kitu kama chuma kinaguswa kisha akasikiya sauti ya mtu ikisema: Una bahati sana wewe, sababu hii nvua isinge likwamisha silaha yangu ulikuwa umekufa leo leo. Mtummishi huyo, hapo hapo akaenda mbio akimushukuru Mungu kwa ile muujiza na akaanza kuomba Mungu amurehemu sababu alikuwa ameanza munungunikia kwa kutojuwa.”
Mfano 2: “Kuna mtumishi wa Mungu mwingine ambaye alialikwa kwenda Ulaya, alipofika kwenye uwanja ya ndege akakuta ndege tayari inaondoka, akasirika na kuwaza mengi; kwanini Mungu anaweza ruhusu mtumishi wake akose ndege. Angali ananungunika pale pale akaona moshi inaanza jitokeza ndani ya libawa ya ndege na hapo hapo ndege hiyo ikateketeya kwa moto na watu wakafa. Kuliko mtumishi anungunike tena, akaanza kushukuru Mungu kwa kuokoa maishi yake na kumuomba Mungu rehema sababu ya ile manunguniko.”
- Lengo la 4: Mungu ana watumiya watumishi wake waaminifu kuwa ishara ya kutukuza jina lake kwa wasio amini. Na hii ni zaidi sana kwa watumishi wa Mungu wa kweli au waaminifu:Mfano 1: Ibrahimu baba yetu wa Imani:
- Utasa: ijapo kuwa ana ahadi ya kuzaa mtoto, ahadi hiyo ikakawiya hadi myaka 25, akapata mtoto akiwa na umuri wa myaka 100 na mkewe Sara akiwa na umuri wa myaka 90 (Mwanzo 17:17);
- Kumutowa mwanawe wa pekee Isaka: (Mwanzo 22:1-18) hii jaribu njo yenye ilimufanya kuwa baba yetu wa Imani tena katika uzao wake mataifa yote ya dunia yatajibarikia.
Mfano 2: Nabii Isaya:
Mungu alimushurutisha avuwe manguo yote muda wa myaka 3 na aende kwa nyumba ya
Israeli yenye kuasi (Isaya 20). Jambo hilo ni
lakusikitisha sana na, si kila mtumishi wa nyakati zetu ambaye anaweza vumilia
hilo jaribu. Mungu, mwenyewe atuwezeshe.
Mfano 3: Nabii Hosea: Nabii huyo ali lazimishwa na Mungu achukuwe mwanamuke kahaba, kwaajili ya utukufu ya Mungu ili kufundisha Israeli taifa la Mungu lenye kuasi (Hosea 1:1-5);
Mfano 4: Nabii Ezekieli: Mungu alimuambia kama atamuondolea kwa pigo moja, mteule wake wa macho; yaani mke wake, tena kaambiwa yeye asiomboleze wala kufanya kilio ili kufundisha mara tena Israeli taifa la Mungu lenye kuasi (Ezekieli 24:15-24);
Mfano 5: Mungu alitaka kusema na mfalme wa Israeli Ahabu, kwa kosa lake lakufanya mapatano na mfalme wa Shamu Ben-hadadi; kuliko kumuanganiza sawasawa na neno la Mungu. Ndipo akatumiya kijana mmoja wa wana wa manabii na kumuambia atafute mtu wa kumupiga mpaka amutiye jeraha kama mtu mwenye kutoka vitani, ...(soma 1 Wafalme. 20:35-43).
Mfano 6: Kuhani Zakaria: Kuhani huyu alikaa kwenye utumishi kwa uaminifu yeye na mke wake Elizabeti; walikuwa wenye haki mbele za Mungu wakiendelea katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama. Alakini hawakukuwa na mtoto, na hilo tatizo halikuwavuruga wala kuwakatisha tamaa katika utumishi wao; hadi Mungu akawakumbuka uzeeni na kuwapa mtoto anaye itwa Yoana mubatizaji, ili awe mutangulizi wa Injili na kazi ya Yesu Kristo hapa duniani (Soma Luka 1:5-7).
Mfano 7: Yesu Kristo mwana wa Mungu: ili mimi na wewe tuokolewe na kusamehewa dhambi zetu, ilibidi Mungu amutowe mwana wake wa pekee kama sadaka ya ondoleo la dhambi na makosa yetu. Aliteswe, akabebeshwa huzuni zetu, aka kataliwa na watu, akazihakiwa katika ya wanyaganyi wa wili, akatemewa mate usoni, akatukanwa na wayahudi, akanyweshwa siki na sifongo; uchi musalabani, akafa kifo cha ayibu kama munyanganyi,... (Yohana 3:16-17; Isaya 53:1-12).
N.B: Ikumbukwe ya kuwa watumishi hao wote tumemaliza kutaja hapo juu, hawakufanya dhambi hata moja kama wengine wanavyo fikiri wanapo ona mtu wa Mungu anajaribiwa.
Shetani jina lake lingine anaitwa Mujaribu, Adui wetu (1 Petr 5:8) Muchonganishi au Mushitaki wetu (Ufunuo 12:10),...
- Alimujaribu mfalme Daudi, kwa kumushawishi afanye hesabu ya wana Waisraeli hata Mungu akakasirika sana na kuazibu hilo taifa kwa tauni ya siku 3 ambayo ili pelekeya vifo vya watu 70.000 (1 Nya. 21:1-15);
- Mtumishi wa Mungu Ayubu: Shetani alimujaribu Ayubu sababu anamupenda sana Mungu na kuogopa dhambi; kwa lengo la kufanya Ayubu amukufuru Mungu wa mbinguni na kukana imani yake (Ayubu 1:6-12);
- Yesu Kristo: Shetani alimujaribu jangwani wakati akiwa kwenye mafungo ya siku 40 muchana na usiku bila kula wala kunywa. Aksanti Mungu sababu Yesu alimushinda kwa kutumiya maneno ya Mungu; tena Roho wa Mungu, alikwisha kumuandaa mapema (soma Luka 4:1-13).
3. TATU: NI MWILI WAKO YENYE KUTAMANI.
Katika kitabu cha Mathayo 26:41-42; tunaona ngisi Yesu alipata shida sababu ya mwili uliokuwa ukimupigiya kelele; hadi kafikiya kuomba Mungu Baba maombi magumu akisema “Ikiwezekana kikombe hiki kinipitiye” yaani mwili ulimujaribu Yesu na kumuonyesha kama si vyepesi na si lazima apitiye mauti; ijapokuwa hiyo ndo lengo lilo tuma Yesu kashuka toka mbinguni kuja kutukomboa kwa njia ya damu na mauti yake; ili anyanganye Shetani kwa njia ya sheria uhalali wote ambao aliokuwa akitumiya kwa kufunga watu wa Mungu kwa njia ya sheria ya zambi na mauti. Sababu mwanadamu alipo asi Mungu, sheria ikatolewa kusema: “... mushahara wa zambi ni mauti ...” (Warumi 6:23). Tena “... Roho itendayo zambi, ndiyo itakayo kufa” au “ [Nafsi itendayo zambi kufa itakufa...]” Soma (Ezekieli 18:20a).
4. SABABU YA 4: NI TAMAA ZITOKAZO KATIKA NAFSI YA MTU
Neno la Mungu kwa kitabu cha 1 Timotheo 6:9-10 “Lakini wale wanaotaka kutajirika huanguka katika majaribu, ndani ya mtego, na katika tamaa nyingi zisizo na maana na ziletazo uharibifu watu katika uharibifu na upotevu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; na wachache, wakiwa wamepagawa, wamefarakana na imani, na kujitupa wenyewe katika mateso mengi”.
Kwenye kitabu cha Habakuki 2:2-3 neno la Mungu linasema: “BWANA akanena nami, akaniambia, Iandike unabii huu, ukaufanye uwe wazi sana katika vibao, ili ausomae apate kuusoma kama maji. Kwa maana ni unabii ambao wakati wake umekwisha kuamriwa, Unaenda mbele muda wake, wala hatasema uongo; ujapokawia, uungojee, kwa sababu haina budi kuja, hakika yatatukia.”
Ninapo soma katika kitabu cha Zaburi 105:17-20 Naona waziwazi ngisi ahadi ya Mungu kuhusu kuinuliwa na kuheshimiwa na ndugu zake sawa sawa na ndoto zake, akiwa nyumbani kwao; Yusufu mwana wa Yakobo ahadi ilimujaribu kabla ndoto zake zivale mwili; tena kwa garama kubwa sana.
6. SITA NA YA MWISHO: KUTUKUZWA, KUPANDISHWA CHEO AU KUINULIWA (Mithali 27:21)
Kitabu hicho cha Mithali ya Sulemani kinaonyesha wazi ngisi “Mtu hujaribiwa kwa sifa zake”.
Kwa hiyo ni lazima kila mtu kuwa mwangalifu anapo sifiwa wala kuinuliwa maishani. Katika kipindi hicho cha sifa au utukufu, waliyo wengi humuchukiza Mungu; sababu Utukufu, Heshima, Uwezo, Mamlaka na Sifa zote ni za Bwana soma: Ufunuo 4:11. Kwa kipindi hiki waliyo wengi, kiburi na sifa nyingi zinatuma wanasahau kumurudishia Mungu sifa, heshima na utukufu wake; na hapo wana sababisha hasira ya Mungu ju yao na hapo Shetani naye anapata nafasi ya kuwashitaki na kuwapiga; sababu sifa ni mulango wa kiroho kama vile imeandikwa kwenye kitabu cha Isaya 60:18 kwa mustari yake ya mwisho. Isaya 60:18
"Jeuri haitasikiwa tena katika nchi yako, Ukiwa na uharibifu hazitakuwa mipakani mwako; Bali utaziita kuta zako, Wokovu, Na malango yako, Sifa."
Umenielewa? Ikiwa hujaelewa, tafadhali fuatana nami tena katika mfululizo mwingine wa somo hili, siku chache zijazo. Tuzidi kuombeana.
Ni mimi katika utumishi wa Kristo.
Pasteur Thaddée Bizy Barhazigirandi
UJUMBE WA NENO LA MUNGU KWA WATU WOTE
Umeletwa kwako na: KANISA "MULIMA WA MAKIMBILIO"
Communauté des Eglises Evangéliques pour toutes les Nations-Unies "C.E.E.N.U"
N° 005, Av. Mulungulungu, Quartier Panzi, Commune d'Ibanda, Ville de Bukavu-RD Congo
à moins de 100 mètres sur RN 2
Adresse mail : tbizyma@gmail.com, thaddemabize@yahoo.fr
Facebook: Thaddée Barhazigirandi; Twitter: @ThaddeeBizimana
Linkedin: https://www.linkedin.com/in/thaddée-bizimana-b79301a8
Commentaires
Enregistrer un commentaire