NYAKATI AMBAZO MUNGU ALIWEKA CHINI YA JUA
USOMI : Muhubiri 3:1-8; 9:11-12 Kwa kumutumikiya Mungu vizuri, ni lazima sana kuzifahamu nyakati hizi ( tatu ) ambazo Mungu alizitenga na kuziweka chini ya juwa; sababu ni lazima zijitokeze kwa kila mtu au mkristo wa kweli kuzishi. Nyakati hizo nazo ni hizi zifuatazo: 1) WAKATI WA SHIDA AU MATATIZO (KIPINDI CHA KUSHUKA): Wakati huu mambo fulanifulani yanajitokeza nayo ni: Magonjwa; kusingiziwa mambo usiyo ya juwa, kukosa kibali na samani mbele za watu, kufukuzwa nyumbani kwa wapangayi, mavalio zaifu au yenye kuchakaa, kukula kwa shida, kuomba msaada kwa ndugu na rafiki bila mafanikio, kukosa kazi, biashara kuhomba, kuibiwa, kuonelewa, kuchekelewa, ... ( Mfano hai: ( Ayubu kwa sura ya kwanza mpaka sura ya 37; Nabii Eliya nyakati za Yezebeli, Yesu Kristo musalabani, na kila mtumishi wa kweli lazima ahonje hicho kipindi .) N.B.1: Wakati huu: Ni lazima mkristo ajuwe kuvumilia mateso, kuacha mihali na lawama na kubaki mwaminifu mbele za Mungu bila kupunguza ne...